Picha: Ray C Aonyesha Muonekano Wake Mpya

Msanii wa muziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ ameonyesha picha yake ya kwanza toka asaidiwe na jeshi la polisi miezi michache iliyopita baada ya kudaiwa kuzidiwa na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Jumatano hii muimbaji huyo aliwaonyesha mashabiki wake muonekano wake mpya hali ambayo imewafanya mashabiki kumtaka kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya kwa kuwa amekuwa akisaidiwa mara kadhaa kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya lakini yeye amekuwa akirudia.

Haya ni baadhi ya maoni ya mashabiki wake.

John_drogba
Jitahidi kivyovyote uache madawa yakulevy binti mzuri weee

dickkami04
Mwanamke wewe nikikumbuka miaka hiyo ya 2003-2006 kipindi ukiwa binti mbichi, juu kimziki, kiuno bila mfupa….. Halafu eti leo hii uko hivi…. Daah!!! Nasikitikaga sana. Kama ungejua dada, ungeolewa zako ukatulia kwa mwanaume yote haya yasingekukuta. Aliyekulaghai akakuingiza humo, si ajabu yeye hayumo… Dah, ona sasa…. Nimemiss sana Ray c wa miaka hiyooooo. Yule wa “Mapenzi yangu”

revish_showbizz_east_africa
No giving up girl u can still stand n become better than the past Ray.just focus n concentrate on ua life keep away fake friends.we still need u you are very important in our community

johari_mtamiza
Mi ningekushauri haya maisha ya kistar achana nayo ndo yanakukost,kubali kuishi maisha mengine kbsa game ishabadilika na umri nao ushaenda mziki wa sasa mgumu,ningekushauri tafuta kazi ya utangazaji ufanye uanze maisha Maya ya kawaida na mungu akikujaalia ukipata mume uolewe uanzishe familia,mziki utakustress urudie tena madawa mziki mgumu wa sasa unahitaji kuwekeza hasa

bongowoodglamour
Usizingue tena sasa utatudisapoint sana km unaona maisha ya uphamous yanakushinda tafta zako mume olewa ishi maisha mengne ya, kumpendeza Allah mana amekupigania sana katika njia zako za maisha other wise tungeshakusahau leo hii @rayc1982 

No comments: