Nay Wa Mitego amchimba mkwara mume wa Shamsa Ford

Nay Wa Mitego ameonekana kumchimba mkwara mwanaume aliyemuowa aliyekuwa mpenzi wake, Shamsa Ford.


Nay na Shamsa walikuwa na mahusiano mwaka 2015 japo mahusiano yao hayakufanikiwa kudumu kwa muda mrefu na kila mtu kufuata njia yake huku wakidai bado ni marafiki wa kawaida.

Kitendo cha kuolewa kwa Shamsa kinaweza kikawa kimemtoa povu rapper huyo kutokana na kipande cha video alichokiweka kwenye mtandao wake wa Instagram na kuandika ujumbe unaosomeka:

TANGAZO TANGAZO TANGAZOOOO😡😡😡
Naskia my #COUSIN Kaolewaaaa Sasa uyo aliyemuoa ipo siku nitampiga Tukio Kama hiiiiiiiiiii😂😂😂🏃🏿🏃🏿🏃🏿🏃🏿
Nina hasiraaaaaaaa🔫🔫😡👹

Shamsa Ford amefanikiwa kufunga ndoa Ijumaa hii na mpenzi wake mfanyabiashara wa maduka ya nguo Rashidi Said aka Chidi Mapenzi. 

No comments: