Je Kuwa MTU Maarufu Kunawezesha Kufanya Kila Kitu Kwenye Tasnia Mbali Mbali?

The industry is too big you cant own it all. The growth of all things depend on focus, persistence and passion and in math we only have 100% to build legacy and less than that to create life style.

Imekuwa jambo la kawaida sana kwenye tasnia yetu kumuona mtu maarufu kutaka kuwa kila kitu katika jamii yetu ukimuuliza kwanini utasikia niliambiwa naweza so nikathubutu. Swali ni je kuwa maarufu kunawezesha kuwa kila kitu katika tasnia? Kama kawaida yetu reference kwa wazungu mtu atatoa mfano mbona Arnold aliweza kuwa mtunishaji misuli bora, mwigizaji bora na Governor hahahaha ukweli ni kwamba kila kitu alikipa nafasi na muda wake hakufanya vyote wakati mmoja. Focus yake kubwa ilikuwa awe bingwa wa dunia katika kutunisha misuli akatwa taji hilo.

Akaingia kwenye sanaa ya maigizo akatusua ulimwengu mzima, kuwa mwanasiasa akafanikiwa pia kuwa Governor wa California jiji kubwa kabisa marekani. Then, katoka kwenye siasa karudi kwenye movies .Amefanikiwa kuacha legacy sababu alitoa muda kwa kila career. @Sammisago ni presenter na blog yake ni moja ya blog kubwa zinazotembelewa na watu wengi.

Lakini cha kushangaza leo anataka kuwa mwanamuziki wakati dunia ya habari ndo kwanza inaanza na wale wenye focus walioanza mapema watafaidika zaidi. @divathebawse #AlaZaRoho ingetikisa Afrika kwa uwezo wako mkubwa lakini umekosa focus, muziki tena? @Idrissultan ni moja ya watu ambao ukisikiliza interview zake unaweza amini upeo wake kuhusu focus aliyonayo damn!

Tunakuwa na mtu zaidi ya @Kevinhart4real duniani. Lakini leo anataka kuwa kila kitu. Unakipindi cha radio ambacho ni masaa saba, unataka uwe bora kwenye comedy na kesho unataka kuwa bora kwenye filamu how many percent do you have as an individual? Is true that one can produce tremendously result when he/she does things partially?

 Leo wewe unachukuliwa kama presenter wakati wengine wanakufahamu kama comedian. Je, itawezekana kuruhusu watu wengine kuwa comedians kupitia wewe and wakaifanya 100%? Huu ni ubinafsi na kwann tunaifinya hii tasnia yetu? @Bongo5 chief editor anataka kutoa mixtape, sasa hivi tutawezaje kupata bloggers wakubwa wa kushindana kimataifa kama wote watakuwa wanamuziki? 

No comments: